|
KUFAHAMU HIFADHI YA JAMII
SW. HIFADHI YA JAMII NI NINI?
JIBU. Kwa mujibu wa maelezo ya Shirika la Kazi
Duniani (ILO) Hifadhi ya Jamii ni hatua ya Kinga
ambayo jamii inatoa kwa wanachama wake, kupitia
mfululizo wa hatua za umma dhidi ya matatizo ya
kiuchumi na kijamii ambayo yanaweza kusababishwa
na kusimamishwa kazi au kupungua kwa kiasi kikubwa
kwa mapato kunakotokana na ugonjwa, uzazi, kuumia
kazini, ukosefu wa ajira, ulemavu, uzee, kifo,
utoaji wa msaada wa huduma za afya kwa familia
zenye watoto.
Mafao ya kulinda kipato yanayotolewa chini ya
programu ya hifadhi ya jamii kwa asili ni fedha.
SW. NINI UTARATIBU MPANGO WA
PENSHENI KWA WATUMISHI WA UMMA NI NINI?
JIBU.Ni utaratibu wa uchangiaji wa pensheni ambao
wanachama huchangia kwa kila mwezi na kupata mafao
yao pale watakapostahili.
SW. MPANGO HUU UNAGHARIMIWAJE?
JIBU: Mpango huu unagharimiwa kwa michango kutoka
kwa waajiri, wafanyakazi na mapato ya vitegauchumi
vinavyomilikiwa na mfuko.
SW: JE, NI KIWANGO GANI CHA MICHANGO
KINATOLEWA?
JIBU: Kila mfanyakazi anatakiwa kutoa mchango
wa 5% ya mshahara wake wa kila mwezi, wakati ambapo
kila mwajiri anatakiwa kutoa mchango wa 15% ya
mshahara wa mfanyakazi wa kila mwezi kwa kuzingatia
mfanyakazi huyo.
SW: JE, MICHANGO INALIPWAJE?
JIBU: Michango ya wafanyakazi inatakiwa kulipwa
katika kipindi cha mwezi mmoja baada ya mwisho
wa mwezi, katika siku ya mwisho ya kipindi cha
kuchangia.
SW: NI NAMNA GANI MICHANGO HIYO
HULIPWA KATIKA MFUKO?
JIBU: Michango hiyo italipwa kwa hundi, fedha
taslimu katika ofisi za PSPF, uhamishaji wa telegrafiki
na njia za kielektroni kwa wataalamu wa Benki
wa PSPF na NMB.
SW: JE, MWANACHAMA ANAWEZA KUTOA
SEHEMU YA MCHANGO WAKE?
JIBU: Hapana, mwanachama hawezi kutoa sehemu
ya michango yake kwa sababu siyo utaratibu wa
kuweka akiba.
Michango inatakiwa kufanywa kwa kipindi cha muda
fulani kilichowekwa ili kuwezesha mpango kulipa
mafao yaliyowekwa dhamana chini ya utaratibu.
Inatambulika, kama sehemu ya malimbikizo ya michango
imetolewa fedha za mpango zitapunguzwa na haitawezekana
kutoa mafao yaliyoahidiwa.
KAZI ZA MFUKO WA PENSHENI KWA
WATUMISHI WA UMMA
SW: MFUKO WA PENSHENI KWA WATUMISHI
WA UMMA (PSPF) HUFANYA NINI?
JIBU: Mfuko hufanya kazi maalumu zifuatazo:
- Kusajili wanachama wote;
- Kusajili waajiri wote;
- Kukusanya michango ya wanachama na kuziweka
pamoja data zinazohusiana na michango;
- Kusimamia na kuwekeza fedha
- Kutunza na kurekebisha kumbukumbu zinazohusu
wanachama.
- Kulipa mafao pale yanapotakiwa.
WANACHAMA WA MFUKO
SW: MWANACHAMA WA MFUKO NI NANI?
JIBU: Wafanyakazi wote wa Serikali Kuu na Wakala
Tendaji walioajiriwa kwa masharti ya pensheni
wanaweza kuwa wanachama wa mfuko ikiwa ni pamoja
na wale waliohamishiwa kwa muda katika taasisi
nyingine.
SW: JE, KAMA MWANACHAMA NITAJISAJILI
WAPI?
JIBU: Wewe kama mwanachama unaweza kujisajili
katika Ofisi za Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi
wa Umma zilizoko katika Jengo la Sukari (Sukari
House) ambalo lipo kona ya Mtaa wa Ohio na Sokoine,
Dar es Salaam au kwa kufanya mipango kati ya mwajiri
na PSPF ambapo zoezi la usajili linaweza kufanyika
katika ofisi za waajiri wakiwepo maofisa wa PSPF.JIBU:
Wewe kama mwanachama unaweza kujisajili katika
Ofisi za Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma
zilizoko katika Jengo la Sukari (Sukari House)
ambalo lipo kona ya Mtaa wa Ohio na Sokoine, Dar
es Salaam au kwa kufanya mipango kati ya mwajiri
na PSPF ambapo zoezi la usajili linaweza kufanyika
katika ofisi za waajiri wakiwepo maofisa wa PSPF.
Kama wewe ni mfanyakazi wa Wakala Tendaji utahitaji
barua ya utambulisho kutoka kwa mwajiri.
SW: JE, UNATAKIWA KUJISAJILI
TENA IKIWA UMEBADILI KAZI AU MWAJIRI?
JIBU: Hapana, unatakiwa kujisajili mara moja
tu. Kama umesajiliwa na una namba ya hundi ya
mshahara au yenye namba ya PSPF, na kama umebadili
kazi, tafadhali mfahamishe mwajiri wako mpya kuhusu
uanachama wako katika mpango na mruhusu aiandike
namba ya hundi ya mshahara wako au namba ya kitambulisho
cha PSPF katika miamala na PSPF.
SW: JE, MTU MWINGINE ANAWEZA
KUTUMIA NAMBA YA CHEKI YAKO YA MSHAHARA?
JIBU: Hapana, Namba ya cheki ya mshahara ni ya
mwanachama pekee na haiwezi kutumika na mtu mwingine
isipokuwa kwa mtu ambaye namba hiyo imetolewa.
Namba ya cheki ya mshahara lazima inakiliwe katika
miamala yote inayohusisha mwanachama na PSPF.
Hakikisha kwamba namba yako sahihi inanakiliwa
katika silipu ya malipo.
Kama mwajiri wako anakata michango yako ya pensheni
ya kila mwezi lakini huna namba ya cheki ya mshahara
au namba ya kitambulisho cha PSPF tafadhali wasiliana
na ofisi za PSPF kwa ushauri.
KUHUSU KUMBUKUMBU BINAFSI
SW: JE, UNATAKIWA KUIFAHAMISHA
PSPF KAMA UMEBADILI JINA?
JIBU: Ndiyo, mwanachama yeyote anayebadili jina
lake anatakiwa kuwasiliana na ofisi za PSPF ili
mabadiliko hayo yaingizwe katika kumbukumbu binafsi
katika PSPF.
SW: JE, UNATAKIWA KUIFAHAMISHA
PSPF PALE UNAPOBADILI ANWANI YAKO?
JIBU: Ndiyo, kama umebadili anwani yako, tafadhali
zifahamishe ofisi za PSPF kwa mabadiliko kuingizwa
katika kumbukumbu binafsi.
SW: JE, UNAWEZA KUBADILI TAREHE
YAKO YA KUZALIWA NA PSPF?
JIBU: Hapana, tarehe ya kuzaliwa haiwezi kubadilishwa.
SW: JE, NI MARA NGAPI MWANACHAMA
ANABADILI WANUFAIKA?
JIBU: Mara nyingi kadri inayowezekana.
MAFAO
SW: KUNA MAFAO GANI KATIKA MPANGO
WA PENSHENI WA PSPF?
JIBU: Mafao ni haya yafuatayo:
SW: NI KITU GANI HUAMUA KIASI
CHA MAFAO?
JIBU: Mpango unahusiana na mshahara, na kiasi
cha mafao kinaamuliwa na muda wa mchango.
HITIMISHO
Kwa maswali zaidi, tafadhali wasiliana na ofisi
za PSPF, ghorofa ya 4, Jengo la Sukari, Kona ya
Mtaa wa Ohio na Sokoine S.L.P. 4843, Dar es Salaam
au kwa simu 022 2120912.

|