|
Kifungu cha 53 (b) cha sheria
Na. 2 ya Mafao ya Watumishi wa Umma wastaafu ya
mwaka 1999 inaeleza moja kati ya kazi kuu za PSPF
ambayo ni "kuwekeza fedha za Mfuko zilizopo."
Ili kufanya kazi hii Mfuko umeanzisha sera ya
usimamizi wa kitegauchumi ambayo ni pana kama
mwongozo wa kuendesha vitegauchumi vyake mbalimbali.
Sera inalenga katika kupata na kutunza kiasi
halisi cha faida katika orodha ya fedha zilizowekwa
kwa faida pamoja na kuendeleza orodha ya vitegauchumi
mbalimbali ambavyo vina uwezo wa kuongoza majukumu
ya Mfuko ya muda mfupi na mrefu katika misingi
endelevu.
Malengo ya Sera
- Kuongeza faida thabiti katika Mfuko na kuwa
na uangalifu mkubwa katika madhara;
- Kuhakikisha kwamba kuna raslimali za kutosha
ili kufikia dhima ya pensheni ya mfuko;
- Kuhakikisha ufaaji wa mali za mfuko kulingana
na mahitaji ya mfuko;
- Sera inalenga katika kupata faida kubwa katika
vitegauchumi ikiwa na
kiasi kidogo cha madhara.
| Usalama: |
PSPF itawekeza mahali
ambapo pana usalama wa Mtaji wa Mfuko. |
| Mazao: |
Faida katika vitegauchumi
lazima iwe inakubalika. |
| Uwezo
wa: |
PSPF itahakikisha
kwamba raslimali za kutosha zinawekwa
Kupata Fedha katika vitegauchumi vya
muda mfupi ili kuwezesha Mfuko
kufikia malengo yake. |
| Matumizi
ya Kiuchumi na kijamii |
Ni katika
maslahi ya Mfuko kuhakikisha kwamba
kiasi
fulani cha fedha kinawekezwa kwa namna
ambayo
kitachangia katika kuboresha hali ya
Elimu na Afya au hali ya maisha ya
Wanachama.
|
|
Upanuzi:
|
Kuhakikisha kwamba
orodha ya fedha zilizowekezwa kwa faida
zinaelekezwa katika hali ya kubadilisha
mazingira. |
|
Orodha ya vitegauchumi
Orodha ya vitegauchumi vya Mfuko imepangwa katika
makundi mawili makubwa; vitegauchumi vya mapato
ya kudumu na vitegauchumi vya mapato ya yasiyo
ya kudumu. Kwa kuzingatia makundi haya, mfuko
umelenga katika kutumia aina za fedha na viwango
vifuatavyo
Aina za fedha na viwango vilivyopendekezwa kwa
mwaka 2002/3 - 2004/5
| Mali
|
Kima
chini* |
Lengo
la kimkakati |
Kima
juu* |
| A:
PATO LA KUDUMU |
|
|
|
| Hawala ya serikali |
15 |
25 |
35 |
| Dhamana
za serikali |
15 |
20 |
30 |
| Amana za muda maalumu
|
10 |
15 |
25 |
| Mikopo ya ushirika |
3 |
5 |
10 |
| Jumla
ndogo |
|
65 |
|
| B:
PATO LISILO LA KUDUMU |
|
|
|
| Hisa: - |
|
|
|
|
Zilizoorodheshwa
|
5 |
10 |
20 |
| Zisizoorodheshwa
|
2 |
8 |
10 |
| Mali halisi |
5 |
10 |
20 |
| Dhamana za shirika |
|
2 |
25 |
| Miundombinu* |
|
5 |
10 |
| Jumla
ndogo |
|
35 |
|
| |
|
|
|
| Jumla
kuu |
|
100 |
|
|
* Jumla ya kimachini na kimajuu hakilingani na
asilimia 100 kwa sababu mabadiliko kutoka katika
mgawanyo wa malengo lazima yafidiwe na kinyume
cha mabadiliko.
** Haya ni maeneo mapya ya vitegauchumi yaliyopendekezwa.

|