|
Menejimenti ya PSPF
Bodi ya Wadhamini inawajibika kwa ajili ya menejimenti
na usimamizi wa Mfuko kufuatana na masharti ya
sheria ya mafao ya Watumishi wa umma wastaafu
Na. 2 ya mwaka 1999. Chini ya Bodi kuna timu ya
Menejimenti ambayo inaongozwa na Mkurugenzi Mkuu,
ambaye anawajibika katika usimamizi wa kila siku
wa Mfuko.
Bodi ya Wadhamini
Mchanganyiko wa wajumbe wa Bodi ni sheria iliyotolewa
chini ya sheria iliyoanzisha Mfuko.
Wajumbe hawa ni pamoja
na:
- Katibu Mkuu wa hazina ambaye ni Mwenyekiti;
- Katibu Mkuu wa Utumishi;
- Mwanasheria Mkuu;
- Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania;
- Katibu Mkuu wa TUGHE;
- Msajili wa Hazina;
- Wajumbe wengine watatu walioteuliwa na Waziri
wa Fedha, wawili wakiwa
- wawakilishi wa TUGHE ambao mmoja wao anatakiwa
kuwa mwanamke, na mwakilishi mmoja kutoka Utumishi.
Menejimenti
Uendeshaji wa kila siku wa mfuko ni jukumu la
Mkurugenzi Mkuu ambaye anatoa ripoti katika Bodi
ya Wadhamini. Mkurugenzi Mkuu husaidiwa na Wakuu
wa Kurugenzi na Vitengo.
Kuna Kurugenzi nne na
vitengo viwili kama ifuatavyo:
- Kurugenzi ya uendeshaji
- Kurugenzi ya Mipango na Vitegauchumi
- Kurugenzi ya Mfumo wa Taarifa
- Kurugenzi ya Fedha na Utawala
- Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
- Kitango cha huduma za Kisheria.
Jedwali la Muundo
Muundo wa Mfuko umeonyeshwa hapa chini:

|