|
UTANGULIZI
Ni utaratibu wa Hifadhi ya Jamii ulioanzishwa
na sheria ya mafao ya watumishi wa Umma wastaafu
Na. 2 ya mwaka 1999 ili kuibadili ile sheria ya
Pensheni, Sura ya 371 ya mwaka 1954.
WAHUSIKA
Wanachama wa Mfuko wa Pensheni kwa watumishi
wa Umma ni Wafanyakazi wa serikali walioajiriwa
Tanzania na wafanyakazi walioajiriwa na Wakala
Tendaji zilizoanzishwa chini ya sheria ya Bunge.
DIRA
Kuwa taasisi imara ya Hifadhi ya Jamii nchini
katika raslimali na mtoaji wa hifadhi ya jamii
anayefaa katika kutoa huduma bora kwa wanachama.
DHAMIRA
Kutoa huduma za hifadhi ya jamii zenye ushindani
kwa wanachama wetu katika hali ya kufaa na ufanisi
kwa kutumia watumishi waliojitoa kwa dhati na
Teknolojia ya inayofaa.
MAADILI
· Kutoa huduma yenye ubora wa hali ya
juu, haraka, kwa ufanisi na heshima;
· Kuwa raia wenye ushirikiano wanaofanya
kazi kwa maslahi ya wanachama wetu;
· Kuwa watumishi wenye wajibu katika fedha
ambazo tumewakabidhi;
· Kukuza uwajibikaji na ubunifu katika
kushirikisha mahitaji ya wanachama wetu.
LENGO
Lengo la Mfuko ni kutoa kwa ajili ya michango
na malipo ya pensheni, kiinua mgongo na mafao
mengine kulingana na huduma kwa wafanyakazi wote
wa serikali wanaostahili Pensheni na wale wote
walioajiriwa na Wakala Tendaji.
UTARATIBU
Mfuko wa pensheni kwa watumishi wa Umma ni utaratibu
wa mafao bayana ya hifadhi ya jamii unaofanya
kazi kwa mujibu wa kanuni za Bima ya Jamii. Wanachama
wa Mfuko wanachangia kwa vipindi na kupata mafao
yao pale watakapostahili.
UGHARIMIAJI
Vyanzo vya mapato ni:-
· Michango ya wafanyakazi ya 5% ya mshahara
msingi
· Michango ya waajiri ya 15% ya mshahara
msingi wa mfanyakazi
· Fedha zinazotokana na vitegauchumi vya
Mfuko
· Fungu la fedha linaloweza kuidhinishwa
na Bunge kwa madhumuni ya Mfuko
· Tathmini ya Mapato na Mtaji vinavyopatikana
kutokana na umilikaji wa mali za Mfuko.
MAFAO YANAYOTOLEWA CHINI YA
UTARATIBU
- Mafao ya Uzeeni
- Mafao ya Ugonjwa
- Mafao ya Kifo na Pensheni kwa wanaobaki
- Mafao ya Msaada wa mazishi
- Mafao ya Kujitoa.
MAFAO
Lengo la Mfuko wa pensheni ni kutoa kipato badili
kwa watu ambao wamepoteza moja kwa moja kipato
chao.
MAFAO YA UZEENI
Ni mafao yanayolipwa kwa mwanachama aliyefikisha
umri miaka 55 au 60 kwa hiari au kwa lazima.
MAFAO YA UGONJWA
Dhana ya ugonjwa inajikita katika kupoteza uwezo
wa kutafuta kipato kutokana na kutokuwa na uwezo.
Tathmini ya ugonjwa itafanywa na Bodi ya kuchunguza
Afya iliyoanzishwa.
MAFAO YA WANAOBAKI
Mafao yanalipwa kwa wategemezi wa marehemu aliyekuwa
mwanachama. Wategemezi hao ni pamoja na mke/mume,
watoto na wazazi wa ofisa aliyefariki. Mafao kwa
wanaobaki hulipwa bila kuathiri sheria za mirathi
zilizopo.
MAFAO YA KIFO
Pale mwanachama anapokufa akiwa katika utumishi
Bodi itampa yule mwakilishi wa kisheria kiasi
chochote cha fedha kisichozidi ama mshahara wake
wa mwaka unaostahili pensheni au kupunguza katika
pensheni ya kiinua mgongo, kama ipo chochote kitakachokuwa
kikubwa.
MSAADA WA MAZISHI
Msaada wa mazishi utatolewa kwa wanafamilia wa
mwanachama aliyefariki kama rambirambi.
MAFAO YA KUJITOA HUZINGATIA:
- NDOA
Hulipwa kwa mwanachama mwanamke anayeolewa kufuatia
kuacha kazi yenye kipato kizuri
- UZAZI
Hulipwa kwa mwanachama mwanamke aliyezaa mtoto
na ameacha kabisa kazi yenye kipato kizuri
- UHAMAJI AU KUKOSA KAZI
Hulipwa kwa mwanachama anayehama au aliyehama
kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
|